
Wahamiaji haramu 16 kutoka nchini somalia wamekamatwa Mkoani morogoro wakiwa wamejificha katika lori la mizigo lililosheni chokaa likitokea jijini dar es salaam kuelekea mkoani mbeya
Kupatikana kwa wahamiaji haramu hao kunatokana na ushirikiano wa wananchi ambao umesaidia kukamatwa kwa wahamiaji hao huku wakidai kuwa baadhi yao walikosa hewa kufuatia kujificha katika mizigo hiyo

Gari lilokuwa limebeba wahamiaji haramu hao likiwa katika kituo cha polisi mkaoni morogoro
Wahamiaji haramu kutoka somalia wamekamatwa Mkoani Morogoro leo .Wahamiaji hao waliokuwa wakisafirishwa katika gari la mizigo lilokuwa limebeba shehena ya chokaaa..
Kwa upande wake afisa uhamiaji mkoa wa Morogoro Hamprey Minja amesema kuwa dereva wa gari hilo amekamatwa na kufikishwa kituo cha polisi ambapo amesema kuwa vyombo vya ulinzi na usalama vimedhibiti kwa kiasi kikubwa maeneo ya mipaka kwa ajili ya kudhibiti matukio ya wahamiaji haramu hali inayopelekea wahamiaji hao kutumia njia nyingine ikiwemo ya kujificha katika magari ya mizigo