
Mkurugenzi wa Sheria na Haki za Binadamu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)na Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu, akiwahutubia wananchi wa mji wa Songea, katika mkutano wa hadhara wa Mabaraza ya Wazi ya chama hicho, kujadili rasimu ya katiba mpya, uliofanyika mjini Songea.

Mmoja wa wakazi wa mji wa Ludewa, Thadey Ngairo, akitoa maoni yake kuhusu katiba mpya, mbele ya Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, wakati wa mkutano wa hadhara wa Mabaraza ya Wazi ya chama hicho wa kujadili katiba mpya mjini Ludewa