http://kariakoodsm.blogspot.com
KARIAKOO BLOG:Kwa Habari Kali Za Mjini | SIASA | BURUDANI | UCHUMI | FASHION | BLOGGER TRICKS | UDAKU | MICHEZO | WASILIANA NA MIMI|0713305567 |urassaombeni@yahoo.com|KWA| MATANGAZO| BABARI| USISITE PIA KUCOMMENT KWENYE HABARI ZETU | <div style='background-color: #de24de;'><a href='http://www.ikiloop.com/' title='link'></a></div>

KILICHOTOKEA LEO MAHAKAMA NI IGUNGA KESI YA KILEWO

KILICHOTOKEA leo Tabora, Mahakama ya Hakimu Mkazi, kesi ya madai ya ugaidi inayomkabili Kamanda Henry Kilewo na wenzake wanne, Henry Kilewo, Evodius Justinian wa Buboka, Oscar Kaijage wa Shinyanga, Seif Magesa Kabuta wa Mwanza, Rajab Daniel Kihawa wa Dodoma.

Washtakiwa waliingia chumba cha mahakama saa 5.00 asubuhi, Hakimu Mkuu Mkazi, Issa Magori, ameingia saa 5.07. Korti ikaanza kwa mawakili wa pande zote mbili kujitambulisha, ambapo upande wa mashtaka ulioongozwa na Wakili Juma Masanja, upande wa utetezi ulikuwa na Wakili Msomi Peter Kibatala na Wakili Emmanuel Musiani.

Hakimu Mkuu Mkazi, Issa Magori akaanza kwa kusema kuwa yale yalikuwa ni maelekezo ya mahakama (si maamuzi?) kwamba ni bahati mbaya kuwa Juni 24, 2013 shauri hilo (namba PI 75 ya mwaka 2013) lilipokelewa mahakamani hapo (Mahakama ya Hakimu Mkazi, Tabora) na mawakili wa pande zote mbili wakafanya mawasilisho yao mahakamani...ni bahati mbaya kwamba mawasilisho hayo yaliandikiwa maelezo hapa kwa ajili ya kufanyiwa maamuzi leo.
Akatoa maelekezo/uamuzi;

Kuhusu shtaka la kwanza, mahakama haina mamlaka ya kusikiliza shauri hilo, yote yaliyofanyika hayakupaswa kufanyika. Hivyo utetezi wowote uliopo unapaswa kuwasilishwa Mahakama Kuu, si katika mahakama ya hakimu mkazi kwani haipaswi kuufanyia maamuzi. Mahakama hiyo haina uwezo wa kuskiliza kesi hiyo.

"Mahakama imeahirishwa hadi baadae...upande wa mashtaka uandae taratibu zingine kwa ajili ya Mahakama Kuu, si hapa," amesema Hakimu Magori, kisha akainuka huku akiacha watu wamepigwa na butwaa, bila kujua hasa kinaendelea. 

Kilikuwa ni kitendo cha dakika 7

Hakimu alionekana kuwa na haraka sana, kiasi kwamba alionekana kusahau masuala kadhaa;

1. Kumuuliza mwendesha mashtaka kama ana lolote la kusema, mathalani kujua kama upelelezi 
wa kesi umekamilika
2. Kutoa uamuzi wowote juu ya shtaka la pili kwenye kesi hiyo, ambalo linahusu kushambulia na kudhuru mwili.

Kwa kweli aliwaacha watu wengi wakiwa puzzled wakiwa hawajui kitu gani cha kufanya, ikiwemo waendesha mashtaka...kwani alifanya kitu kisichokuwa cha kawaida.

Kuhusu marejeo aliyowasilisha Wakili Kibatala

1. Suala la individual calendar; itakumbukwa kuwa kwenye kesi ya Lwakatare, baada ya maamuzi ya Mahakama Kuu kutupilia mbali kesi ya ugaidi, Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ilishindwa kutoa dhamana (iliyokuwa wazi) kwa Lwakatare hadi Hakimu mwenye kesi arudi kutoka likizo. Lakini leo, suala la namna hiyo hiyo limetokea, ambapo 'maelekezo' ya leo yametolewa na hakimu mwingine badala ya hakimu aliyekuwa anasikiliza kesi, Jocktan Rushwela. Haijulikani hadi sasa faili hilo lilihamaje kutoka kwa hakimu wa awali hadi hakimu mwingine.

2. Kujivua madaraka kwa mahakama kwa kushindwa kutoa uamuzi hata kwa mambo yaliyoko 'usoni mwake'

Hoja za awali za upande wa utetezi zilizotolewa Juni 24, wakati kesi iliposikilizwa kwa mara ya kwanza, ambazo ilidhaniwa leo zingetolewa maamuzi ilikuwa ni pamoja na;

1. Mashtaka hayo ya tuhuma za ugaidi, hazina concent ya DPP kwa kadri ya hitaji la sheria katika tuhuma za ugaidi. Katika suala hilo, sheria inasema 'shall'.

2. Charge sheet ya shtaka hilo la ugaidi, haina maelezo yoyote ya kuonesha kuwa kulikuwa na ugaidi au ni tukio la ugaidi (kama ilivyokuwa kwenye kesi ya Lwakatare, mtakumbuka alivyosema Wakili msomi Tundu Lissu wakati ule), kiasi kwamba kwa nini wasishtakiwe kwa kosa jingine la jinai ambalo wanaweza kupata dhamana.

3. Kila mshtakiwa arudishwe na kushtakiwa mahali alikotoka/ alikokamatwa kama ambavyo sheria inaelekeza.

ShareThis